Na Benedict Mayaki, SJ
Watawa wanne wa Kikatoliki walitekwa nyara na watu wasiojulikana katika jimbo la Imo, kusini-mashariki mwa Nigeria siku ya Jumapili.
Watawa hao, Masista Johannes Nwodo, Christabel Echemazu, Liberata Mbamalu na Benita Agu, walikamatwa wakielekea Misa.
Masista waliotekwa nyara ni wa Shirika la Masista wa Yesu Mwokozi ambalo lilitangaza tukio hilo la kusikitisha kupitia taarifa iliyosainiwa na Sr. Zita Ihedoro, Katibu Mkuu.
Sehemu ya taarifa hiyo ilisomeka hivi: “Ndugu na dada wapendwa katika Kristo, ni kwa uchungu mkubwa kwamba tunawajulisha kutekwa nyara kwa dada zetu wanne waliotajwa hapo juu.”
“Tukio la kusikitisha la kutekwa kwao lilitokea eneo la Okigwe-Umulolo asubuhi ya leo muda mfupi baada ya masista hao wakielekea kwenye Misa ya shukrani ya dada yetu.
Kusanyiko liliomba “sala nzito kwa ajili ya kuachiliwa kwao haraka na salama” na kusali Bwana Wetu na Bikira Maria Aliyebarikiwa “kwa ajili ya kuachiliwa bila masharti kwa dada zetu wapendwa.”
Utekaji nyara
Nigeria imeshuhudia kuongezeka kwa matukio ya utekaji nyara katika miezi ya hivi karibuni, huku kukiwa na ripoti za raia kadhaa kutekwa nyara, mara nyingi ili kulipwa fidia, na majambazi na watu wenye silaha katika nchi hiyo yenye watu wengi zaidi barani Afrika.
Utekaji nyara huo pia umewalenga makasisi na viongozi wa kidini wa madhehebu tofauti.
Wiki iliyopita tu, kasisi wa Kikatoliki na mwanaseminari walitekwa nyara kwenye barabara kati ya Okigwe na Umunneochi. Siku mbili baadaye, waliachiliwa.